Sunday, August 19, 2012

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU




 

Ni takribani wiki tatu mfululizo Mchungaji Dr. Ezekiel Mbwilo wa kanisa la TAG Kijitonyama (mwangalizi msaidizi wa section ya Kinondoni) amekuwa na somo la Roho mtakatifu. Roho mtakatifu ni wa muhimu sana katika kanisa na katika maisha ya mwamini. Yesu aliona umuhimu wa Roho mtakatifu ndo maana akasema, hainabudi mimi kuondoka ili aje yule Roho mtakatifu akae kwenu, naye atawafundisha kweli yote. Somo hili ameligawa katika vipengele vingi, kipengele cha kwanza kilikuwa “Umuhimu wa Roho mtakatifu” ambapo alianza kwa kufundisha majina mbalimbali ya Roho mt. Ikifuatiwa na alama/viwakilishi vya Roho mtakatifu.
Katika wiki hii (jumapili hii) Mtumishi wa Mungu aliendeleza somo hili kwa kichwa kinachosema “KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU”
Akihubiri hapa kanisani Mch.Dr. Mbwilo alisema, Karama ni vitendea kazi kutoka kwa Mungu kwenda kwa mwamini kwa ajili ya kufanya kazi ya Mungu. Zipo karama tisa (9) za Roho mtakatifu 1Korith. 12:7-11. Ili kuzielewa vizuri karama hizi, muchungaji alizigawa katika makundi makuu matatu (3) kama ifuatavyo:-
1.Karama mafunuo ambazo ni
 a. Neno la Hekima
 b. Neno la maarifa
 c. karama ya kupambanua Roho

2. Karama za Nguvu
 a. Imani
 b. Karama za miujiza
 c. karama za uponyaji

3. karama za Lugha
 a. Unabii
 b. Aina za lugha
 c. kutafsiri lugha

Karama hizi si kwaajili ya Mchungaji au wazee wa kanisa pekee yake bali ni kwa ajili ya kila mwamini.

A.     KARAMA ZA MAFUNUO
(1)    Neno la hekima; Huu ni ufunuo wa Mungu kwa ajili ya kushughulikia tatizo fulani (mdo 6:1-5; 15:1-15; 1wafalme 3:16-27). Hivyo tunahitaji neno la hekima ili kutatua matatizo yanayotukabili. Karama hii haileti vinyongo, magomvi bali huleta amani, umoja na mapatano. Karama hii pia inasaidia kulielewa neno la Mungu, na inasaidia kujua mambo yajayo. Mfano ufunuo wa Mungu kwa Nuhu juu ya hukumu ya dunia, hivyo kuchukua mtu kuchukua hatua stahiki. Pia inatusaidia kujua mapenzi ya Mungu na mawazo ya Mungu katika maisha yetu.
(2)    Neno la maarifa: karama hii humfunulia mtu kuhusu ukweli au mambo yaliyofichika. Pia inasaidia kuelewa yale yanayo endelea kwenye akili za mwingine mfano ni ile habari ya Anania na Saphira Mdo 5:1-10. Huweka wazi mambo ya siri ya ndani  yaliyofichika kwa wengine. Mfano mzuri ni habari ya mwanamke msamaria Yohana 4:16-19 na habari ya Gehazi na Elisha 2wafalme 5:20-27
(3)    Karama ya kupambanua Roho: Inasaidia kujua ni Roho gani inafanya kazi katika mtu: Je ni roho ya mtu, au ibilisi au Roho ya Mungu (Mdo 8:18-24;13:6-12. Tunahitaji karama hizi ili tuweze kumtumikia Mungu vizuri.

Mpenzi msomaji somo hili litaendelea wiki ijao usipitwe, temebelea blog hii mara kwa mara uweze kufaidika kiroho na kimwili pia. Ebu angalia matukio ya ibada katika picha hapa chini.









Wapendwa wakibubujika ibadani

Mama grace akiwa kazini ibadani akiongoza kusifu na kuabudu

waumini wa TAG kijitonyama wakimwabudu Mungu


Kikundi cha kusifu na Kuabudu kikiwa kazini

Watu wakibubujika katika ibada

Kijitonyama Anointed Singers wakiimba kanisani


Mzee wa zamu(kulia) akiwa na mtafasiri wake wakati wa matangazo

Mch.Dr. Mbwilo (kulia) akihubiri na mtafasiri wake

2 comments: