Monday, August 27, 2012

WASAIDIZI WALIOANDALIWA KUKUSAIDIA UFIKIE HATMA YAKO


Leo ni siku ya pili ya semina, ambapo mtume Israel akiwa na ujumbe maalumu kwa ajili ya Tanzania na kanisa la Tanzania.
Alisisitiza, ili mtu afikie na afanye kile kitu Mungu amempangia katika maisha ni lazima wawepo watu wa kumsaidia.Kwa ufupi ni kwamba kuna mtu ana muujiza wako, na siku mtakapo kutana utapata muujiza wako. Hii ina maana kwamba ili wewe ujue na kutimiza lengo la kwa nini upo duniani ni lazima wawepo watu watakao kusaidia kufikia lengo lako. Kwa bahati mbaya watu wengi hawajui kwamba wanatembea na miujiza ya watu wengine hivyohivyo watu wengi hawajui ni nani mwenye muujiza wake/wao. Kitendawili hiki utakitegua kwa maombi tu. Ni maombi yangu leo Mungu akukutanishe na mtu mwenye muujiza wako.
Akihubiri katika ibada ya jumatatu jioni, mtume Israel akiwa na ujumbe usemao “Msaidizi wa kukusaidia ufikie hatma yako” alisoma katika biblia kitabu cha Yohana 2:2 inayohusu Yesu katika harusi ya kana. Ukiwa ni muujiza wake wa kwanza, aliufanya kwa sababu mama yake ni kama alimlazimisha. Baada ya harusi ile kutindikiwa divai, mama yake Yesu (mariamu) alimwambia Yesu kwamba Divai imeisha, Yesu alimjibu mama yake “nina nini na wewe mwanamke? Tukiangalia hapa hili jibu lilionyesha Yesu hakupenda kufanya muujiza kwa sababu muda wake ulikuwa haujafika. Cha muhimu hapa ni kwamba mwisho wa siku Yesu alifanya muujiza wa kugeuza maji kuwa divai safi na njema. Hapa tunaona mariamu aligundua kwamba Yesu alikuwa na uwezo wa kufanya muujiza. Hivyo alimsaidia Yesu kuanza kufanya miujiza. Sisi leo tunahitaji watu kama mariamu watakao weza kutusaidia kugundua kile kitu tunatakiwa kufanya katika maisha yetu. Ndugu yangu unahitaji mtu akusaidie ufikie leongo lako.
Akihubiri huku mahubiri yakiambatana na maombi alisema kwa kutumia mifano mingi kutoka katika Biblia, Mungu alimwambia Musa atafute watu 70 kwa ajili ya kumsaidia afikie lengo katika maisha kupitia huduma aliyokuwa anaifanya. Esta alimuhitaji Mordekai ili afike ikulu Esta 5:6-8. Wakati wana wa Israeli wakiwa vitani Musa alihitaji watu wa kumsaidia kuitegemeza mikono yake ili israeli ishinde vita, hivyo Haruni na Huri wakaitemeza mikono ya Musa na ushindi wakaupata.
Ndugu yangu msomaji najua unatamani sana kufikia lengo katika maisha yako. Ili haya yatimie unahitaji Mungu akuunganishe na watu wenye miujiza yako, na watakao kusaidia ufikie lengo. Ebu tenga muda wa maombi ili Mungu akuongoze kukutana na watu hao. Mungu akubariki sana sana. 
Mtume Eric Israeli akisikiliza ushuhuda wa mama aliyeponywa na uvimbe tumboni

Watu wengi wakiwa wamejiandaa kutoa ushuhuda wa mambo makubwa Mungu amefanya

Kwaya ya Kijitonyama Anointed wakiimba kanisani

Hapa kila mtu alikuwa anapokea toka kwa Mungu wakati wa maombezi

Mtume Israeli na Mch.Dr. Mbwilo wakiombea watu wenye shida Mbalimbali wakati wa semina


Ibada hii ya leo iliambatana na huduma ya kinabii ambapo watu wengi walibarikiwa sana tena sana.
 
Mpenzi msomaji wangu usikose ibada kama hii kesho,Yesu ni yeye yule jana leo na hata milele.

Sunday, August 26, 2012

TAMBUA HATMA YAKO YA KIUNGU


Ni swali kubwa linalosumbua na kutesa watu wengi sana. Si ajabu kuona na kusikia kwamba watu wengi duniani hawajui kwa nini wapo?, kwa nini walizaliwa? na kwa nini Mungu aliwaumba?. Wengi wanajiuliza kwa nini wanaishi? Lengo la kuishi ni lipi? Hili limekuwa ni fumbo kwa watu wengi. Inasikitisha sana kwani watu wengi wamekufa pasipokufumbua fumbo hili, wengi bado wanahangaika na wengine wamekata tamaa na kuhalalisha mfumo wa maisha wanayoishi wakisema huu ndio mpango wa Mungu. Ebu ungana nami katika somo hili.
Mtume E.Israeli (kulia) na Mch.Dr.Mbwilo (kushoto)

Mtume Eric Okere Israel akihubiri katika ibada ya jumapili asubuhi na ambayo ilikuwa ni siku yake ya kwanza ya kuanza semina kubwa ya uamsho katika kanisa la TAG Kijitonyama, akiwa na ujumbe usemao “TAMBUA HATMA YAKO YA KIUNGU” (Identifying your divine destiny).Alisema kila mtu duniani alizaliwa,aliumbwa ili atimize mambo au jambo fulani katika maisha yake. Akianza ujumbe wake akisoma katika kitabu cha Warumi 8:28-31 alisema, kabla wewe hujazaliwa Mungu alikujua,na kwa makusudi yake amekupangia hatma yako. Tayari aliandika katika kitabu cha kumbukumbu zake juu ya yale utakayotakiwa kuyatimiza katika maisha yako.
Yeremia 1:4-8 tunaona Mungu anamwambia Yeremia akiwa ni mtoto mdogo yasadikiwa kati ya miaka 5 hadi 7 kwamba kabla hujatungwa mimba nalikujua,kabla hujazaliwa nalikuweka kuwa nabii wa mataifa. Mungu alijua vile Yeremia atakavyokuwa hata kabla hajazaliwa. Aliongeza, Mfalme koreshi alitabiriwa kuzaliwa kwake na kazi ya kujenga hekalu atakayoifanya miaka zaidi ya miaka 300 kabla ya kuzaliwa kwake. Hii inaonyesha kwamba hakuna mtu aliyezaliwa duniani kwa bahati mbaya, kila mtu ana jambo la kufanya katika maisha. Inashangaza kwa nini watu wengi hawajui hatma zao katika maisha? Zifuatazo ni sababu zitakazokusaidia kutambua wewe ni nani na nini hatma yako katika maisha.
1.   Ufunuo wa KIMUNGU: ni muhimu sana kumwomba MUNGU ili afungue macho yako/yetu ili uweze kujua wewe ni nani na nini kusudi la Mungu wewe kuwepo duniani kwa maana ya nini unatakiwa kufanya katika maisha yako. Alitoa mfano akisema, mimi niliota ndoto ya kuwa Muhubiri nikiwa na miaka 10 tu. Ndoto hizi zimekuwa halisi kwangu nikiwa mkubwa hivi leo. Yusufu alitambua hatma yake akiwa na miaka 17. Sisi leo tunahitaji Mungu afungue macho yetu kutambua mambo haya makubwa katika maisha yetu.
2.   Mpangilio/mpango wa KIMUNGU: 1samweli 9:1-3 Mungu aliandaa mpangilio wa sauli kuwa mfalme. Mungu aweza kukutengenezea mazingira ya kufikia hatma yako. Jifunze kile Mungu alifanya kwa sauli.
3.   Uvuvio wa KIMUNGU: Unaweza usione maono, ndoto lakini MUNGU akakuongoza kwa uvuvio wake ndani yako na hatimaye ukagundua nini cha kufanya katika maisha yako.
4.   Utafiti: Watu wengi wamegundua hatma yao kwa kusoma Biblia na vitabu vingine vyenye maarifa na vinavyoongeza marifa ya nini cha kufanya. 2Wafalme 22:3-11, baada ya maneno ya Mungu kusomwa mbele yake akagundua nini hatma yake na nini lengo la Mungu la kumfanya kuwa mfalme.
5.   Tangazo la KIMUNGU:Mungu aweza kusema na wewe kwa sauti ya kusikika juu ya nini watakiwa kufanya na kutimiza katika maisha yako. Mungu alisema na Yeremia kwa sauti kwamba amemuweka kuwa nabii wa mataifa.
6.   Muunganiko wa KIMUNGU: yawezekana ikawa vigumu sana wewe peke yako kujua hasa nini hatma yako au jambo gani unatakiwa kufanya katika maisha yako. Ni vizuri kuambatana, au kukaa na watu waliogundua nini cha kufanya katika maisha. Mungu aweza kuku unganisha  na watu wenye hatma zao tayari, ili kupitia hao nawe uweze kujua nini cha kufanya. Yoshua aliunganishwa na Musa hatimaye akawa kiongozi mkubwa kama Musa.
7.   Ufunuo wa kinabii: Mungu aweza kumleta nabii kukueleza nini hatma yako. Kitabu cha Hosea kinasema kwa unabii taifa linapona na haliangamii. Mungu alimtuma Samweli kumtia mafuta Daudi kuwa mfalme.
Ndugu yangu, ni maombi yangu kwa MUNGU akusaidie kugundua hatma na nini cha kufanya katika maisha yako. Wakati mwingine hautoki kimaisha kwa sababu hujajua wewe unatakiwa uwe nani hasa katika dunia hii. Mungu akubariki sana.  
Kwaya ya Kijitonyama Glory Singers wakiimba ibadani

Kwaya ya Kijitonyama Anointed Singers wakiimba kanisani

Watu wakisikiliza kwa makini ujumbe

Mtume akifundisha kwa mfano

Kama kawaida Yesu ni mtamu sana acha nijimimine kwake

Watu wakijimimina mbele za Mungu wao

Sunday, August 19, 2012

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU




 

Ni takribani wiki tatu mfululizo Mchungaji Dr. Ezekiel Mbwilo wa kanisa la TAG Kijitonyama (mwangalizi msaidizi wa section ya Kinondoni) amekuwa na somo la Roho mtakatifu. Roho mtakatifu ni wa muhimu sana katika kanisa na katika maisha ya mwamini. Yesu aliona umuhimu wa Roho mtakatifu ndo maana akasema, hainabudi mimi kuondoka ili aje yule Roho mtakatifu akae kwenu, naye atawafundisha kweli yote. Somo hili ameligawa katika vipengele vingi, kipengele cha kwanza kilikuwa “Umuhimu wa Roho mtakatifu” ambapo alianza kwa kufundisha majina mbalimbali ya Roho mt. Ikifuatiwa na alama/viwakilishi vya Roho mtakatifu.
Katika wiki hii (jumapili hii) Mtumishi wa Mungu aliendeleza somo hili kwa kichwa kinachosema “KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU”
Akihubiri hapa kanisani Mch.Dr. Mbwilo alisema, Karama ni vitendea kazi kutoka kwa Mungu kwenda kwa mwamini kwa ajili ya kufanya kazi ya Mungu. Zipo karama tisa (9) za Roho mtakatifu 1Korith. 12:7-11. Ili kuzielewa vizuri karama hizi, muchungaji alizigawa katika makundi makuu matatu (3) kama ifuatavyo:-
1.Karama mafunuo ambazo ni
 a. Neno la Hekima
 b. Neno la maarifa
 c. karama ya kupambanua Roho

2. Karama za Nguvu
 a. Imani
 b. Karama za miujiza
 c. karama za uponyaji

3. karama za Lugha
 a. Unabii
 b. Aina za lugha
 c. kutafsiri lugha

Karama hizi si kwaajili ya Mchungaji au wazee wa kanisa pekee yake bali ni kwa ajili ya kila mwamini.

A.     KARAMA ZA MAFUNUO
(1)    Neno la hekima; Huu ni ufunuo wa Mungu kwa ajili ya kushughulikia tatizo fulani (mdo 6:1-5; 15:1-15; 1wafalme 3:16-27). Hivyo tunahitaji neno la hekima ili kutatua matatizo yanayotukabili. Karama hii haileti vinyongo, magomvi bali huleta amani, umoja na mapatano. Karama hii pia inasaidia kulielewa neno la Mungu, na inasaidia kujua mambo yajayo. Mfano ufunuo wa Mungu kwa Nuhu juu ya hukumu ya dunia, hivyo kuchukua mtu kuchukua hatua stahiki. Pia inatusaidia kujua mapenzi ya Mungu na mawazo ya Mungu katika maisha yetu.
(2)    Neno la maarifa: karama hii humfunulia mtu kuhusu ukweli au mambo yaliyofichika. Pia inasaidia kuelewa yale yanayo endelea kwenye akili za mwingine mfano ni ile habari ya Anania na Saphira Mdo 5:1-10. Huweka wazi mambo ya siri ya ndani  yaliyofichika kwa wengine. Mfano mzuri ni habari ya mwanamke msamaria Yohana 4:16-19 na habari ya Gehazi na Elisha 2wafalme 5:20-27
(3)    Karama ya kupambanua Roho: Inasaidia kujua ni Roho gani inafanya kazi katika mtu: Je ni roho ya mtu, au ibilisi au Roho ya Mungu (Mdo 8:18-24;13:6-12. Tunahitaji karama hizi ili tuweze kumtumikia Mungu vizuri.

Mpenzi msomaji somo hili litaendelea wiki ijao usipitwe, temebelea blog hii mara kwa mara uweze kufaidika kiroho na kimwili pia. Ebu angalia matukio ya ibada katika picha hapa chini.









Wapendwa wakibubujika ibadani

Mama grace akiwa kazini ibadani akiongoza kusifu na kuabudu

waumini wa TAG kijitonyama wakimwabudu Mungu


Kikundi cha kusifu na Kuabudu kikiwa kazini

Watu wakibubujika katika ibada

Kijitonyama Anointed Singers wakiimba kanisani


Mzee wa zamu(kulia) akiwa na mtafasiri wake wakati wa matangazo

Mch.Dr. Mbwilo (kulia) akihubiri na mtafasiri wake

MKUTANO WA CA'S SURVEY WAFANA

                                       
Ilikuwa ni siku tatu (17-19/8/2012) za miujiza, matendo na kuvuna roho za watu kutoka katika ufalme wa giza na kuwaingiza katika ufalme wa Mungu.Wapendwa wangu tunaishi katika siku za mwisho ambapo ishara moja wapo ya siku za mwisho ni kwamba Injili itahubiriwa ili kila mtu asikie.

Akihubiri katika viwanja vya kanisa la TAG survey, mwinjilisti Shirima akiongea kwa madaha na kufafanua kwa makini kupitia mafunuo na uwezo wa Roho mtakatifu alilinena neno la Mungu kwa ujasiri.
Wakiwahuburia umati mkubwa uliokuja kusikiliza neno la Mungu, alisoma katika Biblia kitabu cha mathayo 1:18-23 alisema. Yesu ni Mungu pamoja na wanadamu, hata kama wewe utakataa lakini kwetu ataendelea kuwa Mungu.Mstari wa 23 unasema; tazama bikira atachukua mimba naye atamzaa mwana wa kiume naye ataitwa Imanueli maana yake ni Mungu pamoja nasi.

Alifafunua kitaalamu na kutoa maana ya jina Yesu=maana yake ni  "atawaokoa watu na dhambi zao" alisisitiza kwa umakini na kusema. Hakuna ugonjwa unaosumbua dunia na watu wake na ambao hauna dawa kama dhambi. Dhambi haina dawa, kama unakataa kamuulize kiongozi wako wa dini kama atakupa jibu. Leo Mungu amenituma kwenu na katika dunia hii kuwatangazia dawa ya dhambi. Dawa ya dhambi ni YESU. Biblia inasema maana atawaokoa watu wake na dhambi zao. Yesu ndo dawa ya dhambi, ukimpokea leo utapona kabisa. Akihubiri kwa kutoa ushuhuda wake alisema, kabla sijaokoka nilikuwa naumwa, tena mtumwa wa dhambi, dhambi iliharibu maisha yangu kiasi kwamba nilikuwa ni maiti inayotembea. Lakini ashukuriwe YESU kwa kuniokoa na leo naonekana ni mtu kati ya watu.

YESU yupo leo akuokoe, damu yake iliyomwagika msalabani ipo hai leo ikutakase maovu yako. Biblia inasema Ukishaa mpokea yesu leo. Tazama ya kale yatapita nawe utakuwa kiumbe kipya. Nakushauri uamue kumpokea YESU awe Bwana na Mwokozi wako. ebu ungana nami katika kuangalia matukia haya ya mkutano katika picha. Mungu akubariki sana.



 KWAYA YA UBUNGO TAG IKIWA KAZINI MKUTANONI


 KWAYA YA VISION IKIWA KIKAZI ZAIDI


KIJITONYAMA ANOINTED SINGERS (TAG K/NYAMA) IKIWA KAZINI


HAPA NI KAZI TU


VIJANA WA YESU WALIOAMUA KUMTUMIKIA MUNGU


WANA WA IBRAHIMU WAKIWA KIKAZI ZAIDI


WATUMISHI WA MUNGU WAKIWA WANASUBIRI


MCHUNGAJI CHAYO WA TAG SURVEY AKIJIANDAA KUMKARIBISHA MUHUBIRI


MWINJILIST NICODEMUS SHIRIMA AKIHUBIRI INJILI YA YESU KRISTO


WATU WAKITUMIA MUDA WAO VIZURI KWA KUSIKILIZA NENO LA MUNGU


Sunday, August 12, 2012

IMANI YA KUTUMIA NDIYO HII


Mathayo 8:5-10; Mistari hii ndiyo ilibeba ujumbe wa leo kanisani "Imani ya kutumia ndiyo hii".Kuna imani za aina nyingi sana, zote zinategemea mazingira, hali, kipato, elimu na maeneo,lakini kuna imani moja tu ya kweli na inayoshinda zote "IMANI KATIKA MUNGU WA KWELI aliyeumba mbingu na nchi. Tukiwa na Imani thabiti katika Mungu hakuna kitu kitatushinda. Imani katika Mungu ikiongezwa au jumulishwa na Neno la Mungu (Biblia) ongeza na Maombi unapata matokea makubwa na mazuri kutoka kwa Mungu wetu.
Maneno haya yalisemwa na mchungaji Anthony kutoka kanisa la TAG Njiro Arusha alipokuwa akihubiri katika la TAG Kijitonyama, Dar es Salaam.Alisema kwa msisitizo ujumbe wake ukiambatana na ushuhuda wake binafsi alisema, Hakika nimemwona Mungu Katika Maisha yangu, hivyo ninazungumza kitu cha kweli na uhakika. Yesu alisema Mkiwa na Imani ndogo kama punje ya haradani mtauambia mlima huu ng'oka ukatupwe baharini. Inasikitisha sana siku za leo tumekuwa na watu wenye uhaba wa Imani thabiti kwa Mungu aliye hai, badala yake watu wametegemea zaidi vitu vya Dunia hii vinavyopita na kuharibika.
Watu wa leo (wakristo wa leo) wanashindwa kujitoa asilimia mia moja kwa Mungu, badala yake wametegemea zaidi kazi zao, vyeo vyao, mali zao, wazazi wao,utajiri wao badala ya kumtegemea Mungu kwa asilimia mia moja.Akitoa ushuhuda wake alisema, tulipokuwa Dhambini tulijitoa sana kwa shetani wengine tulikuwa tunashinda na kukesha vilabuni tukinywa na kulewa, wengine tulitegemea zaidi kazi zetu. Lakini tulipofukuzwa kazi tulikosa pa kukimbilia kwa sababu kazi ndo ilikuwa kila kitiu katika maisha yetu, Vitu vyote vinapita yaani pesa, kazi vyeo na vitu vyote katika dunia hii, Lakini heri mtu yule amtegemeaye Mungu anbaye Imani yake iko kwake.
Nikiwa mchungaji nikichunga kanisa moja hapa Tanzania, ilifika wakati kanisa nililokuwa nikiliongoza wakaniambia kwamba kuanzia leo tutakuwa hatukupi posho. Nilijipa moyo ilihali nikifahamu kuwa  nina kazi nyingine nafanya, kwani nilikuwa nafanya katika ofisi ya Umisheni katika kanisa letu la TAG hivyo mahitaji yangu binafsi na familia bado ningeendelea kuyapata. Ilipofika mwaka 2007 kwa sababu ambazo sizijui huko nako nikasimamishwa. Mpendwa wangu niliumia sana kwani tumaini langu sasa lilikwisha. Hapo ndipo nilipoanza kujifunza kumwamini  na kumtegemea Mungu. Wakati namwomba Mungu afanye njia, ndipo neneo likanitoka "WEWE MUNGU NI AKIBA YANGU" hili neno limekuwa ufungua katika maisha yangu. Toka wakati ule Mungu amenifungulia milango na baraka za Mungu sasa zinamiminika kama mvua maishani mwangu. Mimi kwa sasa siombiombi kwani Mungu amenibariki.Nikutie moyo mkristo mwenzangu hebu tumwamini MUNGU kwa asilimia moa moja, hakika atafanya katika maisha yetu.
Ibada hii kubwa iliambatana na kanisa zima kumpongeza mchungaji kiongozi Dr. Ezekiel Mbwilo ambaye amechanguliwa hivi karibuni kuwa makamu mwangalizi wa section ya Kinondoni. Hebu fuatana nami kwa kuangalia  matukio katika picha. Mungu akubariki sana msomaji wangu.





EMMANUEL RWAKATALE AKIWA KIKAZI ZAIDI

PRAISE & WORSHIP TEAM IKIWA KAZINI KAMA KAWAIDA

PRAISE &WORSHIP TEAM KIUWEPO ZAIDI

WATU WAKIWA WANABUBUJIKA KATIKA UWEPO WA MUNGU

UMEINULIWA JUU SANA JEHOVA

HALELUYAAAAAA YESU NI MTAMU SANA

ROHO MTAKATIFU AKIWEPO NI KUBUBUJIKA TU

YESU YUKO KAZINI,WATU WANAJIMWANGA KWA BABA YAO

WATUMISHI WA MUNGU WAKIWA KAZINI (PEPO TOKA KATIKA JINA LA YESU

GLORY SINGERS WAKIWA KIKAZI ZAIDI

WASHIRIKA WAKIFUATILIA MAHUBIRI KWA MAKINI ZAIDI

MCH. DR.BMWILO NA MKE WAKE PAMOJA NA MGENI WAO REV.ANTHONY

MCH.DR. BWILO AKIJIANDAA KUMKARIBISHA MUHUBIRI WA LEO

REV.ANTHONY AKIWA KIKAZI ZAIDI

MZEE KIONGOZI WA KANISA AKISISITIZA JAMBO MUHIMU SANA

KAMA KAWAIDA MTAWEKA MIKONO JUU YAO NAO WATAPOKEA NGUVU MPYA

MCH.DR.BWILO & MKE WAKE WAKISUBIRI KUPOKEA ZAWADI TOKA KWA KANISA

MCHUNGAJI WA VIJANA AKILIONGOZA KANISA KTK KUTOA ZAWADI 

BABA HONGERA KUWA MWANGALIZI MSAIDIZI,POKEA ZAWADI HII

VIONGOZI WA KANISA WAKISHUHUDIA ZOEZI LA KUMPONGEZA MCHUNGAJI 

KAMA KAWA MSURURU MREEFU TWENDE TUKAMPONGEZE MCHUNGAJI WETU

HONGERA SAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAANA MCHUNGAJI

HATA WATOTO WALIJITOKEZA KUMPONGEZA MUCHUNGAJI WAO

KIJITONYAMA ANOINTED KIKAZI ZAIDI

KIJITONYA ANOINTED SINGERS WAKIWA KAZINI (HATA IMEKUWA......)

AAAAAH  INAPENDEZA KAMA NINI