Sunday, August 12, 2012

IMANI YA KUTUMIA NDIYO HII


Mathayo 8:5-10; Mistari hii ndiyo ilibeba ujumbe wa leo kanisani "Imani ya kutumia ndiyo hii".Kuna imani za aina nyingi sana, zote zinategemea mazingira, hali, kipato, elimu na maeneo,lakini kuna imani moja tu ya kweli na inayoshinda zote "IMANI KATIKA MUNGU WA KWELI aliyeumba mbingu na nchi. Tukiwa na Imani thabiti katika Mungu hakuna kitu kitatushinda. Imani katika Mungu ikiongezwa au jumulishwa na Neno la Mungu (Biblia) ongeza na Maombi unapata matokea makubwa na mazuri kutoka kwa Mungu wetu.
Maneno haya yalisemwa na mchungaji Anthony kutoka kanisa la TAG Njiro Arusha alipokuwa akihubiri katika la TAG Kijitonyama, Dar es Salaam.Alisema kwa msisitizo ujumbe wake ukiambatana na ushuhuda wake binafsi alisema, Hakika nimemwona Mungu Katika Maisha yangu, hivyo ninazungumza kitu cha kweli na uhakika. Yesu alisema Mkiwa na Imani ndogo kama punje ya haradani mtauambia mlima huu ng'oka ukatupwe baharini. Inasikitisha sana siku za leo tumekuwa na watu wenye uhaba wa Imani thabiti kwa Mungu aliye hai, badala yake watu wametegemea zaidi vitu vya Dunia hii vinavyopita na kuharibika.
Watu wa leo (wakristo wa leo) wanashindwa kujitoa asilimia mia moja kwa Mungu, badala yake wametegemea zaidi kazi zao, vyeo vyao, mali zao, wazazi wao,utajiri wao badala ya kumtegemea Mungu kwa asilimia mia moja.Akitoa ushuhuda wake alisema, tulipokuwa Dhambini tulijitoa sana kwa shetani wengine tulikuwa tunashinda na kukesha vilabuni tukinywa na kulewa, wengine tulitegemea zaidi kazi zetu. Lakini tulipofukuzwa kazi tulikosa pa kukimbilia kwa sababu kazi ndo ilikuwa kila kitiu katika maisha yetu, Vitu vyote vinapita yaani pesa, kazi vyeo na vitu vyote katika dunia hii, Lakini heri mtu yule amtegemeaye Mungu anbaye Imani yake iko kwake.
Nikiwa mchungaji nikichunga kanisa moja hapa Tanzania, ilifika wakati kanisa nililokuwa nikiliongoza wakaniambia kwamba kuanzia leo tutakuwa hatukupi posho. Nilijipa moyo ilihali nikifahamu kuwa  nina kazi nyingine nafanya, kwani nilikuwa nafanya katika ofisi ya Umisheni katika kanisa letu la TAG hivyo mahitaji yangu binafsi na familia bado ningeendelea kuyapata. Ilipofika mwaka 2007 kwa sababu ambazo sizijui huko nako nikasimamishwa. Mpendwa wangu niliumia sana kwani tumaini langu sasa lilikwisha. Hapo ndipo nilipoanza kujifunza kumwamini  na kumtegemea Mungu. Wakati namwomba Mungu afanye njia, ndipo neneo likanitoka "WEWE MUNGU NI AKIBA YANGU" hili neno limekuwa ufungua katika maisha yangu. Toka wakati ule Mungu amenifungulia milango na baraka za Mungu sasa zinamiminika kama mvua maishani mwangu. Mimi kwa sasa siombiombi kwani Mungu amenibariki.Nikutie moyo mkristo mwenzangu hebu tumwamini MUNGU kwa asilimia moa moja, hakika atafanya katika maisha yetu.
Ibada hii kubwa iliambatana na kanisa zima kumpongeza mchungaji kiongozi Dr. Ezekiel Mbwilo ambaye amechanguliwa hivi karibuni kuwa makamu mwangalizi wa section ya Kinondoni. Hebu fuatana nami kwa kuangalia  matukio katika picha. Mungu akubariki sana msomaji wangu.





EMMANUEL RWAKATALE AKIWA KIKAZI ZAIDI

PRAISE & WORSHIP TEAM IKIWA KAZINI KAMA KAWAIDA

PRAISE &WORSHIP TEAM KIUWEPO ZAIDI

WATU WAKIWA WANABUBUJIKA KATIKA UWEPO WA MUNGU

UMEINULIWA JUU SANA JEHOVA

HALELUYAAAAAA YESU NI MTAMU SANA

ROHO MTAKATIFU AKIWEPO NI KUBUBUJIKA TU

YESU YUKO KAZINI,WATU WANAJIMWANGA KWA BABA YAO

WATUMISHI WA MUNGU WAKIWA KAZINI (PEPO TOKA KATIKA JINA LA YESU

GLORY SINGERS WAKIWA KIKAZI ZAIDI

WASHIRIKA WAKIFUATILIA MAHUBIRI KWA MAKINI ZAIDI

MCH. DR.BMWILO NA MKE WAKE PAMOJA NA MGENI WAO REV.ANTHONY

MCH.DR. BWILO AKIJIANDAA KUMKARIBISHA MUHUBIRI WA LEO

REV.ANTHONY AKIWA KIKAZI ZAIDI

MZEE KIONGOZI WA KANISA AKISISITIZA JAMBO MUHIMU SANA

KAMA KAWAIDA MTAWEKA MIKONO JUU YAO NAO WATAPOKEA NGUVU MPYA

MCH.DR.BWILO & MKE WAKE WAKISUBIRI KUPOKEA ZAWADI TOKA KWA KANISA

MCHUNGAJI WA VIJANA AKILIONGOZA KANISA KTK KUTOA ZAWADI 

BABA HONGERA KUWA MWANGALIZI MSAIDIZI,POKEA ZAWADI HII

VIONGOZI WA KANISA WAKISHUHUDIA ZOEZI LA KUMPONGEZA MCHUNGAJI 

KAMA KAWA MSURURU MREEFU TWENDE TUKAMPONGEZE MCHUNGAJI WETU

HONGERA SAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAANA MCHUNGAJI

HATA WATOTO WALIJITOKEZA KUMPONGEZA MUCHUNGAJI WAO

KIJITONYAMA ANOINTED KIKAZI ZAIDI

KIJITONYA ANOINTED SINGERS WAKIWA KAZINI (HATA IMEKUWA......)

AAAAAH  INAPENDEZA KAMA NINI

No comments:

Post a Comment