Friday, October 12, 2012

UOVU HUONEKANAJE?



Vitu vingine huonekana na kusababisha hisia za woga, na kutahadharisha. Ebu chukua mfano wa nyoka. Kwa watu wengi, nyoka mara zote hubeba na kuonekana kama ishara ya uovu na hatari. Mimi binafsi siwapendi nyoka. Hutemebea taratibu kwa kujifuta ili wasisikiwe na watu. Kama ungeweza kuniuliza kwa nini, kuna sababu nyingi na nzuri hapa: macho yao madogo ya mduara, matendo/mwendo wao wa kitahadhari, mwendo wao usiogundulika kirahisi, ngozi zao nyororo na zenye utelezi(ndio, najua , magamba)… mwendo wao wa kiupandeupande, na mara zote huonekana wako tayari kushambulia yeyote mbele yao. Lakini kama mwendo na uhatari wao ndo unawafanya kuwa waovu, kwa nini isiwe papa, buibui au hata simba?
Naamini tunaweza kupata jibu zuri kutoka katika bustani za Edeni. Shetani, baada ya kumwasi Mungu na kufukuzwa mbunguni, alichagua kujificha kwa umbo la nyoka. Ikiwa ni matokeo, maelfu ya miaka baadae, bado tunahusisha nyoka na uovu kwa umbo lake la asili.
Nilikuwa nasoma kitabu cha Yakobo ghafula  nikamwelewa nyoka kwa njia ya tofauti sana, baada ya ufahamu ulionijia kwa mfano wa ubaya zaidi ya ulivyofafanuliwa. Kaika Sura ya 3, Yakobo anawahusia wakristo watambue umuhimu wa kuwa makini na maneno yao/kulinda ndimi zao. Alifafanua ulimi wa mwanadamu ni kama:
“...Haujatulia na muovul, umejaa sumu.” (Mstari wa 8)
Lakini unakuwa mbaya zaidi:
“Mara nyingine[ulimi] humsifu Bwana na Baba yetu, na mara zingine tunautumia kuwa laani wote walioumbwa kwa mfano wa Mungu.” (Mstari wa 9)
Je ulishafanya hivyo? Mimi najua nisha wahi kufanya hivyo.
“Na ndivyo baraka na laana zinatoka kwenye kinywa kimoja.” (Mstari wa  10a)
Mara baada ya kusoma mstari huo, sura ya ndimi mbili ndefu za nyoka nilizozitafakari katika mawazo yangu. Biblia inaeleza na kufafanua juu ya mahubiri mabaya kwa njia hii: “Usengenyaji, kuwadharau wengine, kujisifu, kuwanyanyasa wengine, walimu wa uongo, malalamiko na uongo.” Kwa bahati nzuri kila mtu anajua ni mara ngapi ameutumia ulimi wake vibaya akidhani kwamba Mungu hamuoni.
Ni rahisi sana kuufikiria uovu kama uasi, ukali, na wenye sumu kali. Shetani akiwa mwenye ghadhabu na hasira nyingi baada ya kufukuzwa mbinguni, alimwendea Adam na Hawa kwa umbo la Nyoka bila kuogopa. Kwa ujanja mwingi akitumia maneno mazuri yaliyojaa wingi wa ushawishi, huku akiwa amejaa hasira, kinyongo na wivu wa kutaka kumharibu na kumnyang’anya mwanadamu mamlaka aliyopewa na Mungu. Shetani alifanya kwa urahisi kabisa, hakutumia silaha ,uchawi, mazingaumbwe wala nguvu. Alichofanya shetani ni kidogo sana, alitumia silaha ndogo na inayodharauliwa na wengi, “ULIMI”. Kwa ulimi, Shetani aliweza kumjaribu Adam na Hawa kwa swali moja na rahisi,
“Eti Mungu amesema…” (Mwanzo 3:1b)
Kama wakristo, tunafanya kila iliyo juhudi kujilinda na aina zote za uovu. Mauaji, Uzinzi, wizi… lakini bado, tumeshindwa kugundua kwamba kinachotoka vinywani mwetu vinauwezo mkubwa wa kutuletea maumivu, kutujeruhi…na ndiyo, hata kifo.
“Chochote kiujazacho moyo wako ndicho ukisemacho…kwa sababu ndani ya moyo wa mwanadamu hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, aina zote za uasherati, wizi, usengenyaji, na  uongo.” (Mathayo 12:34, 15:18-19)
Tunajilindaje wenyewe na  “umbea, kuwadharau wengine, na walimu wa uongona uongo?” Biblia inasema juu ya yote,
“Linda sana moyo wako, maana ndiko zitokako chemichemi za uzima.” (Mithali 4:23) 
Swali linabakia, Je mtu anawezaje kuulinda moyo wake? Ni kwa kuyakumbuka na kuyatenda yote aliyoyaamuru Mungu na kwa kuwa tayari kufunikwa na nguvu za nane lake kinyume na mipango miovu ya shetani,
“Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi.” (Zaburi 119:11) 

No comments:

Post a Comment