Monday, October 15, 2012

TUNAJIFUNZA NINI KWA YALIYOTOKEA MBAGALA?



Ndugu zangu watanzania, napenda kuchukua fursa hii kuwapa pole Wakristo wote kwa yote yaliyotokea mbagala na kwa uharibifu mkubwa uliofanywa wa nyumba za ibada (makanisa). Najua inauma sana na imeleta usumbufu mkubwa sana miongoni mwetu. Mbali na yote namshukuru Mungu wa Bwana wetu Yesu atupae amani na subira hasa tunapopita katika matatizo makubwa kama haya. Ni maombi yangu kuwa, Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo aendelee kutupa amani, furaha na upendo kwa mapito yote tupitiayo.
Tunapoona haya yote yanatokea, naomba niwakumbushe wakristo wenzangu vitu kadhaa katika misingi na imani ya Kikristo;-

v  Kushindana kwetu sii juu ya damu na nyama bali ni katika falme na pepo wabaya katika ulimwengu wa roho (Waefeso 5).Huu ni wakati wa Kumwomba Mungu na wala si wakati wa kupambana na katika damu na nyama. Katika hali isiyoyakawaida, kuna vitu vingi sana vinaendelea katika ulimwengu wa roho(usioonekana). Unachokiona kinatokea au kinafanyika katika ulimwengu huu unaooneka kimeanzia katika ulimwengu unsioonekana (ulimwengu wa roho).Wakristo wanajua siri hii, hivyo ni wito wangu kwamba, twende katika maombi na tumwite Mungu, na tuharibu kila utendaji na hasa wimbi hili la uharibifu linaloendelea katika nchi yetu. Najua na nina uhakika kwamba litakoma katika jina la YESU.

v  Ukristo umejengwa katika msingi thabiti na imara ambao ni YESU mwenyewe. Yesu alikuja duniani  kumuokoa mwanadamu aliyekuwa amepotea katika dhambi ili amuweke katika ufalme wake. Katika harakati zake za kumuokoa mwanadamu, Yesu hakutumia upanga wala hakumwaga damu. Yesu aliwapenda na anawapenda watu wote. Anawapenda adui zake,na aliwaombea( Mathayo 6,7,8,9).Huu ni mfano mzuri wa kuigwa na  wakristo wote duniani.Pamoja na yote yaliyotokea mbagala, na mabaya yote wanayotendewa wakristo, ni muhimu tukapata msaada wetu toka kwa Mungu. Kulipiza kisasi si juu yetu, Biblia inasema kisasi ni juu ya Mungu mwenyewe.

v  Kunajambo Mungu anasema na kanisa la Tanzania: wakati huu ambapo tumeshuhudia makisa saba (7) yakichomwa na Waislamu Dar es salaam, Mbagala na mengine yaliyochomwa Zanzibar, na Mwanza. Bila shaka Mungu anasema kitu, na anataka atufundishe kitu fulani.Ni maombi yangu kuwa Mungu aseme nasi,naomba kanisa la Mungu Tanzania, litege masikio yake lipate kusikia na kuona kile Mungu anafanya Tanzania.Hakuna kitu ambacho kinaweza kutendeka duniani pasipo Mungu kuwajulisha watumishi wake. Naomba wakristo wenzangu tumwombe Mungu, wako wapi wanawake waombolezaji, nawajitokeze sasa wakaomboleze juu ya Taifa la Tanzania, Juu ya wamama,watoto, wababa, wazee na vijana wa Tanzania.

v  Maombi na subira ndiyo silaha yetu: napenda niwakumbushe wakristo wenzangu kwamba,sisi tunajivunia maombi silaha yetu ya ushindi.Kwa mkristo yeyote na mahali popote alipo lazima atambue kuwa huu ni wakati wa maombi na wala si maneneo tu yasiyokuwa na tija. Kupitia maombi tunaweza kutuliza dhoruba na hali ikawa shwari. Namwamini Mungu anaweza kutuliza hali, na amani ikaendelea kudumu katika Taifa letu. Hii itawezekana tu endapo ufahamu huu utawaingia Wakristo na wakaingia kwenye maombi ya kudhamiria. 2 Nyakati 7:14) inasema ikiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu....................nitasikia toka juu mbinguni nitasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao.

Naomba niwasihi watanzania na wakristo wote Tanzania kuwa na subira na kumwachia Mungu awatetee katika yote wanayopitia.Hakuna mtu aliyeamua kumtegemea na kumwamini Mungu kwa dhati, halafu mwisho wa siku akaaibika au Mungu akamwacha mtu huyo, haiwezekani.
POLISI WAKIWASHIKA BAADHI YA WALIOSHIRKI KATIKA VURUGU

VITU VIKIWA VIMECHOMWA BARABARANI

MOJA LA GARI LA POLISI KATIKA KUWADHIBITI WAANDAMANAJI

POLISI WAKIDUMISHA USALAMA KATIKA ENEO LA TUKIO

MOJA KATI YA MAKANISA SABA LIKICHOMWA MOTO

WAISLAMU WAKIWA KITUO CHA POLISI WAKIDAI WAPEWE MTUHUMIWA WAO

MLANGO WA KANISA UKIWA UMEHARIBIWA KWA MAWE

WACHUNGAJI NA WAUMINI WAKIANGALIA UHARIBIFU ULIOFANYWA KANISANI

MABENCHI YA KANISA YAKIWA YAMEVUNJWA KABISA

MABENCHI YAKIWA YAMEVUNJWAVUNJWA

MIMBARI IKIONEKANA KUCHOMWA MOTO KABISA

HUU NI UHARIBIFU MKUBWA

BAADHI YA VYOMBO VYA MUZIKI VIKIWA VIMEUNGUZWA

MADIRISHA NA MILANGO IKIWA IMEHARIBIWA KABISA

OFISI YA MCHUNGAJI IKIWA IMEHARIBIWA KABISA

BAADHI YA WACHUNGAJI WAKISUBIRI TAARIFA KUTOKA POLISI

BAADHI YA WAUMINI WAKIOMBA MUNGU

VYOMBO VYA MUZIKI VIKIWA VIMECHOMWA MOTO

WAUMINI WAKITAFAKARI KILICHOTOKEA KANISANI KWAO

MOJAWAPO LA GARI LILILOHARIBIWA VIBAYA KABISA



KUSHOTO NI MSIKITI AMBAO WAISLAMU WALIJIKUSANYA NA KULIVAMIA KANISA UPANDE WA KULIA NA KUFANYA UHARIBIFU MKUBWA

No comments:

Post a Comment