Monday, September 3, 2012

KONGAMANO KUBWA LAFANA SINZA REFUGEE CENTER


Ni kongamano kubwa la aina yake lililojaa miujiza na ishara nyingi za Roho mtakatifu lililofanyika katika kanisa la TAG Sinza Refugee Center.Watumishi wa Mungu waliovikwa nguvu za Mungu na madhihirisho ya nguvu za Roho mtakatifu, wakiongozwa na Mch. Seiko sheyo (Mwenyeji) pamoja na Mch. Joseph Marwa (mgeni muhubiri na katibu wa jimbo la zanzibar) walihubiri kwa nguvu za Mungu. Sinza imetetemeshwa kwa nguvu za Mungu, hakika Mungu anawatumia watumishi wake kukionya na kukielekeza kizazi cha leo kimrudie Mungu na kulifundisha kanisa la Mungu kusimama na kuitenda kazi ya Mungu.
Akihubiri kwa nguvu za Roho mtakatifu Mch.Joseph Marwa kutoka Zanzibar alisema, Kizazi cha leo kinahitaji madhihirisho ya nguvu za Mungu na wala si maneno matupu. Tunapoujulisha ulimwengu juu ya nguvu za Mungu wetu lazima nguvu zake  zionekane kuwa ushuhuda kwa watu wote. Akihubiri kutoka kitabu cha cha Waamuzi 2:6-10, kwamba kikainuka kizazi kingine nyuma yao ambacho hakikumjua Mungu..........Alisisitiza kizazi chetu kinahitaji kujulishwa juu ya Mungu wa Mbinguni mwenye nguvu na uwezo wa ajabu. Akifundisha kwa mifano alisema kulipita vizazi vinne kama ifuatavyo;-
(1)         Kizazi cha Musa; Kiliona bahari ikipasuka mbele yao, kilikula kwale jagwani, kilikula mana jangwani iliokuwa ikidondoka kila siku toka mbinguni,kilisikia sauti ya Mungu lakini hakikumwamini Mungu, na Mungu akaadhimia kukiangamiza jangwani badala yake wakapona Yoshua na Kalebu.
(2)         Kizazi cha Yoshua na kalebu; kizazi hiki kilitumia uzoefu wa mababu zao, ingawaje Mungu alitaka kitumie uzoefu mpya kwa kufundishwa na Mungu mwenyewe. Hivyo Mungu alijifunua upya kwa kizazi hiki.
(3)         Kizazi cha wazee: hichi ni kizazi kilichozaliwa jangwani na ambacho kiliingia katika nchi ya ahadi.
(4)         Kikainuka kizazi kipya; Biblia inasema baada ya vizazi vyote vya kwanza kupita kikainuka kizazi kipya kisicho mjua Mungu. Kizazi hiki kilikuwa na matatizo yafuatayo (1) Hakikumjua Mungu (2) Hakikuwahi kuiona ile kazi Mungu alifanya wakati wote walipokuwa Jangwani. Kizazi hiki kinafanana na kizazi cha leo.
Tunahitaji Mungu atendae kazi katika kizazi cha leo, tunahitaji watumishi wa Mungu wenye nguvu za Mungu watende kazi ya Mungu kwa madhihirisho ya Roho mtakatifu kuwa ushuhuda kwa watu wote duniani. Kizazi cha sasa kinahitaji Matendo makuu na miujiza na ishara na wala sio maneno tu.Biblia ina sema “Yesu kristo ni yeye yule jana leo na hata milele”
Rafiki yangu msomaji kama bado hujampa Yesu maisha yako amua leo akuokoe akufanye mtoto wake hakika ya kale yatapita nawe utakuwa kiumbe kipya.Ebu tazama matukio katika picha jinsi kongamano lilivyo kuwa.
Hii ndo madhabahu ya TAG Sinza Refugee Center

Kikundi cha kusifu na kuabudu kikiwa kazini siku ya Kongamano

Kikundi cha kusifu na kuabudu kama kawa

Kiongozi wa kusifu na kuabudu akiwaongoza watu katika kumsifu Mungu

Mwinjilisti Christopher akiwa kikazi zaidi madhabahuni pa Bwana Yesu

Christopher akiwa kazini na kikundi cha kusifu na kuabudu

Mch.Sote (booster) akiwa amejaa nguvu za Mungu tayari kwa kazi

Umati wa watu wakiwa ktk Ibada ya kusifu

Watu wakiserebuka wakati wa kipindi cha kusifu

Haya sasa hapo bariki amen, bariki amen!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kama kawa, watu wote bariki Amen!!!!!!bariki Amen!!!!!

Mwinjilisti Christopher akiwa kazini zaidi

Mch. seiko (mwenyeji) na mch. sote wakiimba yekelekele aaah! zambe wa moyo

Kwaya ya wenyeji wakiimba wakati wa kongamano

Kwaya ya Kijitonyama Anointed wakiimba wakati wa kongamano

Watu wakisikiliza kwa makini wakati K

Kwaya ya Revival magomeni wakiimba wakati wa kongamano

Kijana amani wa kwaya ya Revival magomeni akiwa kazini

Kikombe cha babu akiimba wakati wa kongamano akisaidiana na christopher

Christopher akiimba wimbo wa "saa imefika ya kubarikiwa"

Watu wakibarikiwa na wimbo wa Saa imefika ya kubarikiwa

Watu wakiserebuka wakati christopher akiimba



Mch. Joseph Marwa akihubiri kwa nguvu za Mungu wakati wa kongamano

Mch. Marwa akifundisha kwa mifano aina 4 za vizazi

Ilikuwa ni kazi kwelikweli

Mch. marwa akiwa tayari kufanya maombezi kwa watu wenye shida mbalimbali

Maombezi yakifanyika katika jina la YESU KRISTO

Jopo la watumishi wa Mungu wakifanya maombezi kwa watu wenye shida katika jina la YESU

Tumepewa jina moja la YESU! katika jina la YESU uwe mzima!

Yesu akiwa kazini kwa madhihirisho ya Roho mtakatifu



Funguka katika jina la YESU!

Pokeeni nguvu za Mungu

Watu wakijimimina katika uwepo wa Mungu


Mwinjilisti Christopher akiwa kwenye mitambo

Mama uwe mzima katika Jina la YESU

Funguka katika jina la YESU


4 comments:

  1. Mungu wetu ni mwema sana, ibada hii ilikuwa ya kupendeza kwa maana ya kuinua vijana katika kuelekea kuifanya kazi ya Bwana ikiambatana na miujiza mingi.
    Naona watu wlijaa Roho kwa WIngi sana Mungu ni mwema.

    ReplyDelete
  2. Mh na wakumbuka hawa watumishi walipakwa mafua ya kumsifu Bwana na kuhubiri kwa njia ya uimbaji.
    Mr. Christopher na Ernesty a.k.a Kikombe cha babu.

    ReplyDelete
  3. ujumbe ulionigusa ni kuwa vijana leo tunahitaji kuwa na nguvu za Mungu ili Ulimwengu uone kazi za Yesu na wapate kumwamini Mungu. kazi ni kwa vijana kumtafuta Mungu kutenga Muda wa kusoma Neno la MUNGU ilikujua yale ambayo Mungu alitenda, Macho yetu yAtiwe nuru kumwona Mungu kwa namna ya uungu wake KIUTENDAJI ZAIDI.

    ReplyDelete